Friday, March 8, 2013

ODAMA, MUSA BANZI KIMENUKA


Stori: Hamida Hassan
PRODYUZA mkongwe Bongo, Musa Banzi amegombana na staa wa sinema za Kibongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ kwa kumtosa kuweka picha yake kwenye kalenda aliyoiandaa.
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichoomba hifadhi ya jina, Odama ameandaa kalenda na kuisambaza mitaani ambapo imesheheni mastaa kibao isipokuwa Musa ambaye alitoa mchango mkubwa kumtoa kisanaa na kusababisha prodyuza huyo amchukie.
Alipotafutwa Odama kuhusu ishu hiyo, alikiri kutokea kwa kutoelewana kati yao lakini wameyazungumza na kuyamaliza.
“Alisahaulika bahati mbaya kwa sababu idea ilikuja ghafla nikasahau kuweka picha ya Musa lakini hata hivyo tulishalizungumza suala hilo na sasa tunafanya kazi yetu ya Close The River,” alisema Odama.

No comments:

Post a Comment