BONDIA wa Marekani, Floyd Mayweather amemchapa mpinzani wake raia wa Ufilipino, Manny Pacquiao kwa pointi katika mpambano wao wa karne uliopigwa Ukumbi wa MGM Grand jijini Las Vegas leo asubuhi.
Majaji wa mpambano huo uliokuwa wa raundi 12 wamempa ushindi Mayweather kwa alama hizi: 118-110, 116-112, 116-112.
Baada ya pambano la leo, Mayweather ameshinda mapambano yake yote 48 aliyopigana hakiwa bado hajapoteza mchezo wowote.
No comments:
Post a Comment