Sunday, September 30, 2012

Maduka na ofisi zafungwa Kismayo

 30 Septemba, 2012 - Saa 15:28 GMT

Wakaazi wa mji wenye bandari wa Kismayo, kusini mwa Somalia, wanasema bado mji huo haudhibitiwi na mtu yoyote.
Mapigano kuania Kismayo
Siku ya Ijumaa vikosi vya Kenya na serikali ya Somalia vilifika kaskazini ya mji huo na kupelekea wapiganaji wa Kiislamu wa al-Shabaab kuondoka.
Mizinga ilisikika usiku, lakini vikosi hivo bado viko nje ya mji.
Kuna taarifa kuwa wazee kadha wameuliwa na watu wenye silaha na shule na maduka karibu yote yamefungwa.
Kismayo ilikuwa ngome kubwa ya mwisho ya al-Shabaab, ambako wakiweza kuagiza silaha kutoka nchi za nje na kupokea pato kwa kuwatoza kodi wafanya-biashara.

No comments:

Post a Comment