Tayari mpaka sasa wasanii wa
kundi la vichekesho la ORIJINO KOMEDI TBC1 Mpoki, Joti na Masanja
wanafanya muziki, kama hautambui naomba nikufahamishe kwamba Wakuvanga
nae ameongezeka kwenye list ya wanaofanya muziki.
Amezungumza na millardayo.com
na hapa namkariri aliyoyasema kwamba “mimi nafanya Komedi na ukiwa
unafanya komedi una uwanja mpana unaweza kuwaigiza wanamuziki kwa hiyo
nimetimiza vile vitu ambavyo vinahitajika kuwa comedian, nina sauti za
Chidi Benz, Fid Q, Roma na wengine, sasa hivi sijatoa album
nimeintroduce single inaitwa Angwisa, nilikua na sababu ya msingi ya
kuifanya iwe ya kwanza kwenye album yangu, album na video viko tayari na
vitasambazwa kuanzia tarehe 25 december 2012″
Kuhusu aina ya muziki
alioufanya, Wakuvanga amesema “nimefanya Ragga, bolingo.. nyimbo
nilizoimba zinafanana na wapagani, watu wa kanisa, ni nyimbo ambazo
hazitukani, hazimtaji Yesu lakini inakidhi mahitaji ya watanzania”
Sentensi ya mwisho kutoka kwa
Vengu ninayomkariri anasema “mimi nimewahi kujaribu vitu vingi kwenye
maisha yangu, zamani tulikua tunajifunza kurap nilikua mchora katuni,
nilijaribu vitu vingi nikajaribu na comedy na katika comedy ndio
nimeweza kuwa comedian, sio mwanamuziki lakini muziki niliwahi kujaribu
sikufanikiwa hii nafanya ni katika kutimiza ndoto zangu”
No comments:
Post a Comment