Sunday, April 6, 2014

WAGOMBEA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE WAPIGA KURA ZAO

 Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia tiketi ya CCM, Ndugu Ridhiwani Kikwete akihakiki taarifa zake kabla ya kupiga kura kwenye kituo cha Ofisi ya Mtendaji Kata namba 3 Bwilingu, Chalinze.
Aziza ambaye ni mtoto wa mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM, Ndugu Ridhiwani Kikwete akimsaidia baba yake kuweka kura kwenye sanduku la kura. Ridhiwani alipigia kura yake kwenye kata ya Bwilingu.

 Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chadema, Ndugu Mathayo Torongey akizungumza na baadhi ya mawakala alipotembelea kituo cha Ofisi ya Mtendaji Kata namba 1, Bwilingu.

 Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha AFP, Ndugu Ramadhani Mgaya akizungumza na waandishi wa habari nje ya kituo cha Ofisi ya Mtendaji Kata namba 1 na kusema kuwa chama chake kitakubali matokea yeyote na pia kama watashindwa watajipanga kwa ajili ya uchaguzi ujao mwaka 2015.
Mkurugenzi wa Uchaguzi Jimbo la Chalinze, Ndugu Samuel Salianga akizungumza na waandishi wa habari nje ya kituo cha Ofisi ya Mtendaji Kata Bwilingu na kutoa tathmini ya jinsi zoezi linavyoendelea na kufafanua mambo mbalimbali yanayohusu uhalali wa wagombea kupiga kura popote ndani ya jimbo la uchaguzi.
(PICHA ZOTE NA FATHER BLOG)

No comments:

Post a Comment