Friday, April 5, 2013

HE! MASOGANGE AJIANIKA


Stori: Hamida Hassan
Mwanadashosti muuza nyago kwenye filamu na video za wasanii wa Bongo Fleva, Agness Gerald ‘Masogange’ amejianika kimahaba zaidi mtandaoni akiwa na mchumba’ke ambaye ni staa wa filamu za Kibongo, Evans Komu, Ijumaa lina mzigo kamili.
Baada ya ukimya wa muda mrefu tangu iliponaswa video yake chafu, mwanzoni mwa wiki hii Masogange alitupia picha hizo zisizo na maadili ya Kitanzania kwenye akaunti yake ya Mtandao wa Instagram na kuibua mjadala mzito.
Katika picha hizo zilizowekwa kwenye akaunti hiyo iliyokuwa na jina la ‘aggnesfineassgirl’ kabla ya kufutwa, msichana huyo wa mjini anaonekana akiwa na jamaa yake chumbani, wakiwa wamezama kwenye mahaba mazito.
“Duh! Hii sasa ni too much (imezidi) na haikubaliki kwenye jamii, waachwe wafanye wazungu lakini siyo sisi tuliostaraabika,” ilisomeka sehemu ya maoni mengi katika mitandao tofauti ya kijamii juu ya kitendo hicho kisichokubalika.
Ili kupata undani wa kuvuja kwa picha hizo au sababu za Masogange kujianika ovyo kimahaba mtandaoni, Ijumaa lilimwendea hewani mrembo huyo kupitia kilongalonga chake lakini hakupatikana. 

No comments:

Post a Comment